SPORTS

 

Idris Sultan Amtundika Mimba Wema Sepetu























Mshindi wa Big Brother Afrika, Idris Sultan amepasua jipu kuhusu uhusiano wake na Wema Sepetu ambao umekuwa ukizua utata kila siku huku mashabiki wao wakiubatiza majina mbalimbali. Idris ameweka wazi kuhusu hali ya uhusiano wao na namna anavyomchukulia Wema Sepetu kama mkewe.  Kwa mujibu wa maelezo yake, yeye na mrembo huyo wanatarajia kupata mtoto ingawa bado hawajafahamu jinsi ya..

 

 

 

Diamond Amwaga Machozi Ukumbini


Mbongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, amejikuta akiangua kilio kama mtoto mdogo na kuwashangaza watu kufuatia mashabiki wake kumtaka awaimbie ‘akapela’ ya wimbo wake mpya wa Utanipenda.

Tukio hilo ambao bado limo midomoni mwa mashabiki wake, lilijiri usiku wa kuamkia Boxing Day (Desemba 26, 2015) ndani ya ‘Uwanja wa Taifa wa Burudani’ Dar Live jijini Dar ambapo nyota huyo alikuwa akikamua jukwaani na shoo ya nguvu iliyopewa jina la Funga Mwaka Concert.

Dakika chache kabla Diamond hajamwaga chozi, mashabiki wake walimuomba aimbe ‘akapela’ ya wimbo huo mpya.

Wakati akiimba akapela hiyo, mashabiki wake, bila kificho, walimwambia anajitabiria ‘kufulia’ kwani wimbo huo una kila alama za yeye kumaliza gemu la Bongo Fleva vibaya.

Hata hivyo, licha ya mashabiki kumpasulia hivyo, baadhi yao walianza kulia wakionekana kuguswa na mashairi ya wimbo huo hali iliyosababisha Diamond naye aanze kulia na kushindwa kuendelea kuuimba wimbo huo.

Kufuatia hali hiyo, dada yake kwa upande wa baba yake, Abdul Jumaa, Mwanahawa Abdul ‘Queen Darleen’ alimfuata jukwaani na kumtoa huku akimfunika na kitambaa cha bendera ya taifa ambacho pia dada huyo alikitumia kumfutia machozi kaka yake huyo.

Diamond alipelekwa nyuma ya jukwaa ambako ukiachia mbali yeye Queen Darleen, meneja wake, Hamis Taletale ‘Babu Tale’ naye alitumia nguvu ya ziada kumbembeleza staa huyo huku akimwambia anawapa wasiwasi mashabiki wake. Kwa hiyo anyamaze.

Licha ya Babu Tale kutumia hekima ya kibabubabu, bado Diamond aliendelea kulia, safari hii kwa uchungu zaidi na kujiinamia huku akikataa kutulizwa wala kuambiwa maneno yoyote yanayoonekana ‘kama’ yana busara ndani yake.

“Huna sababu ya kuendelea kulia ndugu yangu kwani kufulia au kuendelea kuwa na mali ni neema na msimamo wa Mungu. Hakuna binadamu anayeweza kumshusha mwenzake kama Mungu hajapanga kuwa hivyo,” alisema Babu Tale lakini Diamond hakumsikiliza.

Diamond alinyamaza mwenyewe baadaye kufuatia mawasiliano ndani ya ubongo wake kumwambia ‘umelia sana kijana, imetosha sasa’!

Kilio hicho, kilimaliza shoo hiyo kwani Diamond hakurudi tena jukwaani baada ya kukamua nyimbo zake kibao na kuwafanya mashabiki wake kuiweka siku hiyo katika kumbukumbu.

Wimbo ulimuliiza Diamond huu hapa
Mpekuzi blog

 

 

Kwa mashabiki wa Liverpool hizi sio habari njema kwa staa wao Daniel Sturridge …

Hizi haziwezi kuwa taarifa njema kwa mshambuliaji wa kimataifa wa Uingereza anayeichezea klabu ya Liverpool Daniel Sturridge ambaye hakupata nafasi ya kucheza wala kukaa benchi katika mchezo wa michuano ya UEFA Europa League usiku wa November 26 dhidi ya Bordeaux  katika uwanja wao wa nyumbani wa Anfield.
Staa huyo wa Liverpool ambaye alikuwa nje ya uwanja toka October 4 baada ya kuwa majeruhi na kulazimika kuwa nje ya kwa muda, alikuwa akitazamiwa kucheza mchezo wa Europa League usiku wa November 26 ila stori mpya ni kuwa nyota huyo ameshindwa kurejea uwanjani baada ya kuonekana bado alikuwa na tatizo.
Daniel Sturridge mwenye umri wa miaka 26 ambaye alikuwa akilalamika kuhisi maumivu katika mguu wake, amepata nafasi ya kucheza mechi tatu pekee msimu huu na 18 kwa mwaka 2015, alifunga magoli mawili katika ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Aston Villa September 26 lakini bado hajapata nafasi ya kucheza chini ya kocha mpya Jurgen Klopp.

 Full Time ya Liverpool Vs Bordeaux Europa League Nov 26 2015

Usiku wa November 25 ilipigwa michezo ya mechi za klabu Bingwa barani Ulaya, lakini usiku wa November 26 ilikuwa ni zamu ya muendelezo wa mechi za michuano ya UEFA Europa League, klabu ya Liverpool ambayo inashiriki michuano hiyo ilikuwa mwenyeji wa klabu ya Bordeaux katika dimba la Anfield.
Liverpool ambao wapo chini ya kocha wao mpya mjerumani Jurgen Klopp waliingia katika dimba lao la nyumbani wakiwa na kumbukumbu nzuri ya ushindi wa goli 4-1 kutoka katika mchezo wao wa Ligi Kuu Uingereza iliyocheza dhidi ya Man City katika uwanja wa Etihad, Liverpool ilianza kwa kuruhusu kufungwa goli na Bordeaux dakika ya 33 kupitia kwa Henri Saivet.
Livepool ambao kwa muda mrefu walikuwa wanaongoza kumiliki mpira, walifanikiwa kusawazisha goli hilo kwa mkwaju wa penati dakika ya 38 kupitia kwa James Milner, Liverpool waliongeza mashambulizi na dakika ya 45 Christian Benteke akapachika goli la pili na kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa goli 2-1. Licha ya Bordeaux walionesha jitihada za kutaka kusawazisha goli kipindi cha pili, mchezo ulimazika kwa Liverpool kuibuka na ushindi wa goli 2-1.

No comments:

Post a Comment